Covenant Protestant Reformed Church
Bookmark and Share

Imani Ya Nike

 

Ninamwamini Mungu mumoja, Baba Mwenyezi,

Muumba wa mbingu na dunia, 

na vitu vyote vinavyoonekana na visivyoonekana.

 

Ninamwamini Bwana mumoja, Yesu Kristo,

Mwana wa pekee wa Mungu,

amezaliwa na Baba mbele ya kuwa ulimwengu, 

Mungu kutoka Mungu, Nuru kwa Nuru,

Mungu kweli kwa Mungu kweli,

amezaliwa, hakuumbwa,

Mwenye umungu mumoja na Baba.

Vitu vyote viliumbwa naye.

Alishuka toka mbinguni,

kwa ajili ya sisi watu,

na kwa ajili ya wokovu wetu;

alitwaa mwili kwa tendo la Roho Mutakatifu,

katika Bikira Maria,

akawa mutu.

Akasulibiwa kwa ajili yetu,

wakati wa Pontio Pilato,

akateswa, akazikwa,

Akafufuka kisha siku tatu,

kama ilivyoandikwa;

akapanda mbinguni,

anakaa kwa mukono wa kuume kwa Baba.

Ndipo atarudi kwa utukufu,

kuwahukumu wazima na wafu,

na ufalme wake hautakuwa na mwisho.

 

Ninamwamini Roho Mutakatifu,

Bwana na Mutoa uzima, 

aliyetoka kwa Baba na Mwana,

anayeabudiwa na kutukuzwa,

pamoja na Baba na Mwana,

aliyesema kwa manabii.

 

Ninaamini Kanisa, moja, takatifu, katolika,

lililotoka kwa Mitume.

Ninasadikia ubatizo mumoja

kwa kuondolewa kwa zambi. 

Ninangojea ufufuko wa wafu

na uzima wa milele utakaokuja.  Amina.